MchipukoSanaa

Anjella ft. Harmonize – kama

Baada ya harmonize kumtambulisha rasmi, anjella ambaye ndiye msanii mpya wa label ya konde gang ameachia nyimbo mpya ” Kama” aliyomshirikisha boss wake ambaye ni harmonize.

Kazi hii yao imeachiwa mda mfupi baada ya msanii kutoka wasafi rayvanny kuzindua label yake mpya kwa lengo la kuwasaidia wasanii chipukizi.

Anjella ft. Harmonize – kama, sio nyimbo ya msanii huyu ya kwanza kwani hapo awali waliachia nyimbo nyengine kwa jina all night. Anjella ana sauti nzuri na kama hizi nyimbo yuandika mwenyewe basi anajua sana.

Kwa sasa atakuwa na mwenzake ibra na wasanii wengine ndani ya konde gang. Swali letu ni je, ataweza kufikia kiwango cha zuchu ambaye ni msanii wa kike ndani ya label ya wasafi? Letu hapa mwangaza ni jicho tu na kama kutakuwa na lipya tokeo, basi tutakuwa watu wa kwanza kuwajulisha.

Soma hii pia ( historia ya Zuchu)

Tazama Anjella ft. Harmonize – kama  kwa Mara ya kwanza hapa mwangaza news

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *