Princess Tiffah azidi kushangaza wengi
Princess Tiffah ambaye ni mtoto wa diamond platnumz na zari Hassan azidi kushangaza wengi. Watu wengi humininika kwa page yake ya Instagram maana wanajua anacho kipost kinapendeza.
Kama mtoto huyu hayuko na mamake wakicheza, basi Yuko sehemu akiongea na babake diamond platnumz ama akilalamikia babake kwa kutopokea simu zake.
Katika video aliyo post mamake, wengi waliipenda sana. Katika hiyo video, princess Tiffah alionekana akiongoza maombi.
Hata kama princess Tiffah ana miaka kidogo, mambo anayoyafanya ni kama ya mtu mzima. Hupenda kuombea mamake, ndugu zake na hata wanyama wa nyumbani.
Kabla ya kumaliza maombi, princess Tiffah anaonekana akiomba anachokihitaji maishani mwake na pia kwa marafiki zake.
Soma hii pia ( uhusiano wa Mama Dangote na princess Tiffah)
” Asante mungu kwa chakula, nashukuru kwa kila mtu akiwemo babangu, mamangu na ndugu zangu……
Asante kwa hizi mbwa zetu…zidi kutulinda.. tunakupenda sana na nahitaji kuwa rafiki yako….tuonane baadae…” Aliandika Tiffah.