HistoriaMaisha

Historia Ya Rose Muhando

Rose Mhando ni msanii wa muziki wa injili kutoka Tanzania. Alizaliwa mwaka 1976 Wilaya ya Kilosa, Mkoa wa Morogoro katika familia ya Kiislamu. Alikuwa akisoma Madrasa baada ya shule lakini alibadili dini na kuwa Mkristo baada ya kuona maono ya Yesu Kristo. Rose ni mama wa watoto watatu na anajulikana kama Malkia wa muziki wa injili Afrika Mashariki. Zidi kuwa nasi ili ujue zaidi maisha na Historia Ya Rose Muhando

Maisha ya Rose Muhando

Alipokuwa na umri wa miaka tisa, alipatwa na ugonjwa usiojulikana uliomfanya alale kitandani kwa miaka mitatu. Alipona baada ya kuona maono ya Yesu Kristo. Rose Mhando ni mama wa watoto watatu. Alianza kazi yake ya muziki kama mwalimu wa kwaya katika Kanisa la Anglikana la Chimuli mjini Dodoma. Baadaye alianza kuimba nyimbo zake za injili na akawa msanii maarufu na mshindi wa tuzo mbalimbali

Nyimbo Za Rose Muhando

Rose Mhando ana nyimbo nyingi za injili ambazo zimepata umaarufu na kupendwa na watu wengi. Nyimbo yake ya juzi ambayo imekuwa gumzo kote afrika yajulikana Kama Secret Agenda. Baadhi ya nyimbo zake ni:

  • Waache Waende
  • Secret Agenda
  • Kama Mbaya Mbaya
  • Wanyamazishe
  • Yesu Karibu Kwangu
  • Nibebe
  • Ndivyo Ulivyo

Familia Ya Rose Muhando

Familia Ya Rose Muhando

Rose Muhando ni mama wa watoto watatu. Hata hivyo, haijulikani kama ana mume au la. Kuna uvumi kwamba alikuwa na uhusiano na mchungaji wa Kenya, lakini hakuna uthibitisho

Nyimbo Ya Secret Agenda ya Rose Muhando

Secret Agenda ni nyimbo moja kati ya nyimbo kumi na mbili katika albamu mpya ya Rose Muhando iliyotolewa mwaka 2022. Nyimbo hiyo inahusu jinsi Mungu anavyowalinda watumishi wake kutokana na mipango mibaya ya maadui zao

Masomo na Safari ya Mziki

Haijulikani kama Rose Muhando alimaliza masomo yake au la. Hata hivyo, alianza kazi yake ya muziki kama mwalimu wa kwaya katika Kanisa la Anglikana la Chimuli mjini Dodoma

Utajiri wa Rose Muhando

Utajiri wake unakadiriwa kuwa kati ya dola milioni 1 hadi 5. Rose Muhando ameshinda tuzo mbalimbali kama vile Skiza Ring Back Tone of the Year mwaka 2011 na Best Singer in Tanzania mwaka 2009

Ni hayo tu kwa sasa kuhusiana na Historia Ya Rose Muhando. Natumai umejifunza mengi. Zidi kufuatilia habari zetu hapa Mwangaza kwani tuna mengi zaidi ya kuwajuza na kama kawaida kabla ya kuwajuza chochote huwa tunafanya utafiti dhabiti

Pia soma, Historia ya Jay Melody

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *