Grace Msalame aongelea kuhusu ujauzito wake
Grace Msalame ambaye ni mtangazaji, hivi karibuni atakuwa mama wa watoto wa tatu. Habari hizi aliziweka wazi kwenye mtandao huku akieka picha akipapasa tumbo lake linaloonyesha kuwa ni mja mzito.
Grace Msalame amesema kwamba uja uzito wake kwa sasa umetimiza miezi sita. Alionekana na furaha sana kumkaribisha mtoto wake wa tatu.
Grace ni mama wa mapacha na kwa sasa mapacha hao wako na miaka tisa. Majina yao kamili ni zawadi na Raha ila kwa mitandao hupenda kuwaita ZaRa. Mapacha hawa aliwapata na mchumba wake wa hapo awali kwa jina Paul Ndichu.
Paul Ndichu alioa tena mwanamke kwa jina Evaline Momanyi na wako na mtoto mmoja naye. Paul Ndichu ni kakake Edward Ndichu ambaye ni mmewe Janet Mbugua.
Grace Msalame juzi kwenye mahojiano, alisema hakuwa ameolewa na Paul Ndichu na wawili hawa walipata watoto nje ya ndoa.
Hadi sasa, Grace Msalame hajaeka wazi ni nani anahusika na uja uzito wake ila anaonekana kama mwenye ako naye kwa sasa huenda wakafunga naye pingu za maisha.
Soma hii pia (vipindi vipya ndani ya maisha magic plus)