Jovial Ft. mejja – Pakua
Mejja amekuwa mfalme wa colabo. Jovial Ft. mejja – Pakua ni nyimbo iliyotayarishwa na umakini zaidi kuanzia audio mpaka video. Jovial naye ameonekana kuongeza bidii kila uchao na kazi hii mpya kaitendea haki
Jovial ni mzaliwa wa Mombasa japo siku hizi amehamia Nairobi. Msanii huyu Anajulikana nchini Kenya na afrika mashariki kwa jumla. Sauti yake imeenda shule na kwa kweli anajua anachokifanya. Na Kama jovial kaandika mwenyewe hii nyimbo, basi ametisha sana
Mejja naye amekuwa mfalme wa colabo. Kumbuka miezi kadhaa iliyopita alifanya colabo na femi one, “utawezana” iliyozua gumzo afrika nzima. Video ya pakua imetayarishwa na crystal prime ambaye siku hizi anajiita Director Dolls. Director huyu anapenda anachokifanya na ni gwiji sana katika kazi ya kuongoza na kutayarisha music video.
Kama hujatazama video mpya ya Jovial Ft. mejja – Pakua, Basi bonyeza link ifuatayo upate burudani halisi
Tazama hii pia ( susumila ft. Nadia)
https://youtu.be/cF89wycSPyU